Waumini walipata nafasi ya kujikumbusha ujumbe wa Arubaini - msisitizo wa upendo, kujitolea na mshikamano wa Kiislamu -sambamba na kushiriki kwa vitendo katika kuokoa maisha kupitia uchangiaji damu.

19 Agosti 2025 - 22:00

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Waumini kutoka vituo vya Ngare Nairobi, Mwangaza na Matadi, wilayani Siha mkoani Kilimanjaro, wakiongozwa na Sheikh Said Shekigenda -Mkuu wa Kanda hizo- waliadhimisha kumbukumbu ya Arubaini ya Mashahidi wa Karbala mnamo tarehe 15 Agosti 2025.

Waumini wa Wilaya ya Siha waadhimisha Arubaini ya Imam Hussein (as) na Mashahidi wa Karbala kwa Ibada na Uchangiaji Damu +Picha

Waumini wa Wilaya ya Siha waadhimisha Arubaini ya Imam Hussein (as) na Mashahidi wa Karbala kwa Ibada na Uchangiaji Damu +Picha

Sehemu ya maadhimisho hayo ilihusisha kampeni ya uchangiaji damu katika Zahanati ya Ngare Nairobi, ikiwa ni sehemu ya kuenzi thamani ya kujitolea kwa Imam Hussein (a.s) na mashahidi wenzake.

Katika majlis hiyo, Sheikh Ma’amun Husein Adamu alikuwa mzungumzaji mkuu ambapo alitoa mada kuhusu “Fadhila za Kumtembelea (Kumzuru) Abā ‘Abdillāh al-Hussein (a.s)”.

Waumini wa Wilaya ya Siha waadhimisha Arubaini ya Imam Hussein (as) na Mashahidi wa Karbala kwa Ibada na Uchangiaji Damu +Picha

Waumini walipata nafasi ya kujikumbusha ujumbe wa Arubaini – msisitizo wa upendo, kujitolea na mshikamano wa Kiislamu – sambamba na kushiriki kwa vitendo katika kuokoa maisha kupitia uchangiaji damu.

Waumini wa Wilaya ya Siha waadhimisha Arubaini ya Imam Hussein (as) na Mashahidi wa Karbala kwa Ibada na Uchangiaji Damu +Picha

Your Comment

You are replying to: .
captcha